- Kishazi:
Kishazi ni nini?
Kishazi ni aina ya
tungo chenye kitenzi ambacho huweza kujitosheleza au kutojitosheleza. Yaani
kuweza kuleta maana inayotarajiwa au hakiwezi kusimama peke yake kikaweza
kuleta maana kamili inayotarajiwa. Mfano;
v Mzee
analima.
v Mtoto
aliyekuja jana…
Katika mifano hiyo
tunakuwa kwamba, tungo ya kwanza imeweza kujitosheleza kimaana lakini katika
tungo ya pili haikuweza kujitosheleza kimaana kwani haikuweza kuekeza huyo
mtoto aliyekuja jana amefanya kitu gani.
Sifa
za kishazi:
ü Kishazi
ni lazima kiwe kitenzi.
ü Baadhi
ya vishazi huweza kujitegemea hata kama sentensi ikiondolewa katika muktadha wa
sentensi kuu.
ü Vishazi
vingi hasa vishanzi huru huwa na kiima dhahiri.
ü Vishazi,
hasa vishazi huru kwa kawaida huwa na kitenzi kimoja kikuu.
Aina
za vishazi:
Kuna aina kuu mbili za
vishzi. Navyo ni:-
a.
Vishazi huru.
b.
Vishazi tegemezi.
Vishazi huru:
Vishazi huru ni vishazi
ambavyo hujitosheleza kimaana na kuwa na vitenzi vikuu. Yaani vishazi huru
huweza kusimama peke yake na kutoa ujumbe kamili usiohitaji maelezo. Mfano;
Ø Mzee
aliyekuja ameshaondoka.
Ø Gari
tulilokuja nalo limeondika.
Sifa za vishazi huru:
Ø Kishazi
huru huwa na hadhi ya sentensi sahili
Ø Havina
urejeshi.
Ø Hujitosheleza
katika kuleta maana ya tungo.
Ø Huwa
na vitenzi vikuu.
Vishazi tegemezi:
Vishazi tegemezi ni
aina ya vishazi ambavyo huwa na kitenzi kisaidizi ambacho hakikamilishi ujumbe.
Kwa kawaida vishazi tegemezi hutegemea vishazi huru ili kuweza kukamilisha
maana halisi ya ujumbe uliokusudiw
a. Mfano;
v Mbuzi
aliyeumia mguu…
v Maji
yaliyomwagika…
v Watoto
waliopotea…
Sifa za vishazi
tegemezi:
ü Hutawaliwa
na urejeshi.
ü Huweza
kuondoshwa katika sentensi bila kuharibu maana kamili ya sentensi mzima.
ü Huweza
kutangukiwa au kufuatwa na vishazi huru.
No comments:
Post a Comment