SENTENSI


Sentensi:

Senensi ni nini?

Sentensi ni kifungu cha maneno chenye kiima na kiarifu ambacho huleta maana iliyokamili. Kwa kawaida sentensi huwa na miundo mikuu miwili. Miundo hiyo ni:-

v  Kiima.

v  Kiarifu.

Kiima:

Kiima ni sehemu ya sentensi ambayo hukaliwa na mtenda au mtendwa wa jambo linaloelezwa. Katika sentensi, kiima kutokea kyshoto mwa kitenzi. Mfano;

Ø  Mama anapika.

Ø  Embe zimeharibika.

Vipashio vya kiima:

ü  Nomino peke yake. Mfano;

Mtoto anacheza.

ü  Nomino na kivumishi. Mfano;

Watoto wote ni watundu.

ü  Nomino na Nomino. Mfano;

Baba na mama wanakima.

ü  Kivumishi na Kiwakilishi. Mfano;

Vile vyao viliokotwa kuke.

Kiarifu:

Kiarifu ni sehemu ya sentensi ambayo hukaliwa na kitenzi ambacho huarifu tendo lilivofanywa, linavyofanywa au liutakavyofanywa. Kiarifu ndiyo sehemu muhimu zaidi katika sentensi kwani huweza husimama bila kiima. Mfano;

                        Juma anacheza mpira.

                        Watoto wanaimba vizuri.

Vipashio vya kiarifu:

ü  Kitenzi kikuu peke yake. Mfano;

Anasoma gazeti.

Anakwenda sokoni.

ü  Kitenzi kisaidizi na kitenzi kikuu. Mfano;

Wahida alikuwa anasomesha.

Walimu walikuwa na kikao.

Aina za sentensi:

Kuna aina kuu nne (4) za sentensi. Nazo ni;

ü  Sentensi sahili: Ni aina ya sentensi ambayo hujengwa na kishazi huru kimoja. Mfano;

Ali analima shamba

ü  Sentensi changamano: Ni aina ya sentensi ambayo hujengwa na kishazi huru kimoja au zaidi na kishazi tegemezi kimoja au zaidi. Mfano;

Nyumbu aliyepigwa risasi amekimbia.

Mbwa aliyepata kichaa muogope.

ü  Sentensi ambatano: Ni aina ya sentensi ambayo huundwa na sentensi mbili au zaidi. Mfamo;

Mama anapika na baba anafua.

Magazeti huuzwa na watu hununua.

ü  Sentensi shurutia: Ni aina ya sentensi ambayo ina vishazi tegemezi viwiwli au zaidi ambavyo utegemezi wake hutokana na mofimu –nge, -ngali, -ngeli, ki n.k. zinazojitokeza katika kitenzi. Mfano;

Angelijibu maswali yote, angelifaulu mitihani yake.

Akija tutaondoka.

Akinipa nitampenda.

No comments:

Post a Comment

<marquee>YALIYOMO</marquee>

MAANA YA TUNGO AINA ZA TUNGO TUNGO NENO TUNGO KIRAI TUNGO KISHAZI SENTENSI